Facebook Fan Page Computer Tutorials News Blogging Internet Latest Posts

Today is:

Berry Black kupakua ngoma mpya makonelah records

Berry Black kupakua ngoma mpya makonelah records

You are Here: Home > News > Berry Black kupakua ngoma mpya makonelah records

Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Berry Black almaarufu Mfalme wa Zenji Fleva, amerekodi ngoma mpya katika studio za Makonelah Records mjini Unguja. Berry Black ameamua kumshirikisha msanii mwenzake, Samir katika nyimbo hiyo ambayo taarifa zinasema kuwa ataitoa muda wowote kwa mashabiki wake, utengenezaji wake ukishakamilika.

Kama nilivyosema hapo juu, ni kwamba ngoma hiyo inatengenezewa katika studio za Makonelah Records zilizopo mjini unguja (Zanzabr).

Naimani mashabiki wa Berry Black mtafurahi kwa ujio wa ngoma hiyo, kutokana na ukweli kwamba Berry amekuwa akijitahidi kushirikisha wasanii wenzake, kitu ambacho kinafanya nyimbo zake ziwe na ladha tofauti-tofauti, na kuleta burudani murua kwa wapenzi wa muziki wa kizazi kipya.

Aidha, nikizungumza na mmiliki, mwendeshaji na pia producer mkuu wa studio za Makonelah Records Bw. Musa Makonelah, aliniambia kuwa nyimbo hiyo anaifanyia 'Mixing' (Anaiweka katika hali sawa ili ikae mkao wa kinyimbo kamili na yenye kusikilizika), na kwamba akishamaliza majukumu yake katika nyimbo hiyo kama producer, ataikabidhi kwa Berry ili iweze kuingia sokoni.

Kila la kheri Berry Black!

Makonelah records ni miongoni mwa studio kongwe za muziki visiwani Zanzibar zinazofanya vizuri kunako 'Game' la muziki wa kizazi kipya nchini. Ipo maeneo ya Mchina Mwanzo, ikiongozwa na Mr. Musa Makonelah. Kwa taarifa zaidi unaweza kuwatafuta kupitia tovuti yao ya http://makonelahrecordz.blogspot.com/

Picha ya Msanii Berry Black

You may also like this!

R. One wa Keroh apania kurudi tena kwenye gemu la muziki wa bongo flava
Baada ya msanii wa bongo flavour Rashid A. Rashid a.k.a R. One wa Keroh, kukaa kimya kwa muda mrefu kimuziki, ameamua...

Mbunge wa Nzega, Dr. Hamis kigwangalla asema hatowasusia fisi bucha!
Mbunge anayeshikilia jimbo la Nzega mjini, katika wilaya ya Nzega mkoani Tabora, Dr. Hamis Kigwangalla, ametoa...

Maalim Seif amewatia kitasa wanaotaka kuua ukawa!
Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu mkuu wa chama cha CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, amesema mipango inayofanywa...

Advertisement!

About this blog's Author!

Mpiga Kabeya is a Computer teacher. He also enjoys coding professionally, highly experienced on HTML, JavaScript, Php, Css, VB Script, etc. He is also a professional graphics designer as well as.....
Check him on Google+!

Advertisement!